• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Waziri Gwajima awataka Wajasiriamali kujiunga na majukwaa ya wanawake ili kutangaza biashara zao

Tarehe iliyowekwa: September 11th, 2023

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima amewataka wajasiriamali kujiunga na majukwaa ya wanawake lengo likiwa ni kurasimisha biashara zao ili waweze kufanya biashara kwa wigo mpana zaidi.

Mhe. Dkt. Gwajima ameyasema hayo tarehe 11 Septemba, 2023 katika ufunguzi wa Maonesho ya Wajasiriamali yaliyoandaliwa na Taasisi ya CRDB Bank kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Ya Ilala yenye kauli mbiu isemayo ‘Asante Rais Samia biashara zimefunguka’ lengo likiwa ni kutoa muamko kwa wajasiriamali ili waweze kuchangamkia fursa mbalimbali zinazopatikana baada ya kujiunga na majukwaa mbalimbali yanayoambatana na elimu ya ujasiriamali.

Aidha Dkt. Gwajima ameongeza kuwa ili kwenda na wakati na kupata fursa zinazotokea katika mchakato mzima wa ununuzi ni vyema wajasiriamali wakarasimisha biashara zao na kujiunga na majukwaa ya wanawake kwani Sekta binafsi zinaonesha mchango mkubwa wa kuwakwamua wanawake na vijana ili kukuza uchumi wa taifa letu.

“Nipende kumshukuru Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzanzia Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuamua kuunda Wizara hii ili ishirikiane na ninyi kwani kuna faida nyingi kwenye majukwaa hivyo wanawake mnyanyuane mfike kwenye majukwaa fursa zipo muachane na mikopo yenye riba kubwa nendeni ‘Imbeju’ kuna fursa.” Ameeleza Dkt. Gwajima.

Vilevile Dkt. Gwajima ametoa shukrani zake kwa CRDB Bank na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ilala kwa kuanzisha maonesho haya endelevu huku akiahidi kuitangaza programu yao ya ‘imbeju’ wakati anapokua kwenye mikutano yake mbalimbali lengo likiwa ni kuhakikisha wajasiriamali wote wanapata elimu za kuboresha bidhaa zao na kupata masoko zaidi.

Akiongea kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Edward Mpogolo ameeleza kuwa “Katika kuwawezesha wananchi kiuchumi, Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ilala kupitia Idara ya Maendeleo ya Jamii tulishirikiana na CRDB Bank ambapo walitueleza juu ya Programu ya Imbeju huku na sisi tukiwa na Asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri hivyo tuliona ni vyema kuungana kuanziasha maonesho haya lengo likiwa ni kutengeneza masoko kwa wajasiriamali wetu na kuwapa elimu juu ya ujasiriamali. Hivyo tunawashukuru sana CRDB Bank foundation kwa kuanzisha programu ya Imbeju ambayo imekua chachu ya wajasiriamali kujipatia mikopo mbalimbali kwaajili ya kuendeleza biashara zao na kujikwamua kiuchumi.”

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Ndg. Abdulmajid Mussa Nsekela ameleza kuwa katika kuwakwamua wanawake na vijana Wajasiriamali elfu 65 wamefikiwa na programu ya imbeju huku mikopo ya zaidi ya shilingi Milion 200 zikitolewa kwa baadhi ya vikundi vya wajasiriamali.

Aidha katika maonesho hayo mikopo mbalimbali ilikabidhiwa kwa baadhi ya wajasiriamali ikiwepo mikopo ya bajaji, pikipiki pamoja na fedha taslimu.

Maonesho haya ni bure na yatafanyika kwa siku tatu kuanzia leo tarehe 11 hadi 13 ambapo wananchi watapewa elimu mbalimbali juu ya ujasiriamali na jinsi ya kutafuta masoko ndani ya nchi na nje ya nchi.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.