• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

RC Makalla Aongoza Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Mkoa wa Dar es Salaam

Tarehe iliyowekwa: March 8th, 2023

Kila Tarehe 08 Machi Taifa linaadhimisha siku ya Wanawake Duniani ambapo Leo Machi 08, 2023 maadhimisho hayo katika Mkoa wa Dar es Salaam yameweza kuadhimishwa katika viwanja Vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam huku mgeni rasmi akiwa ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Amos Makalla.

Katika maadhimisho hayo yenye kauli mbiu isemayo "UBUNIFU NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA NI CHACHU KATIKA KULETA USAWA WA KIJINSIA" yameweza kubeba sura ya Kongamano la Wanawake na Fursa za Kiuchumi, yaliwapa nafasi kina mama na vikundi mbalimbali vya ujasiriamali kushiriki, kuonyesha bidhaa zao, na kuuza bidhaa hizo.

Akiongea katika maadhimisho hayo Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe.Amos Makalla amesema “Kwanza kabisa napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa Rais wa Jamuhuri ya Muunguno wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan kwa kuweza kuwawezesha Wanawake kiuchumi kupitia mikopo ya Halmashauri kwani Billioni 13.9 zimeweza kutolewa kwaaajili ya kusaidia vikundi vya Wanawake,Vijana pamoja na watu wenye ulemavu ikiwa bilioni 6.1 wamepewa Wanawake huku bilioni 5.9 zikielekezwa katika vikundi vya Vijana na bilioni 1.8 zikielekezwa katika vikundi vya watu wenye ulemavu ambapo takribani vikundi 1243 vimeweza kunufaika na mikopo hiyo ikiwa vikundi 69 ni vya wanawake vukundi 428 ni za vijana na vikundi 126 vikiwa ni vya watu wenye ulemavu hivyo natoa wito kwa wananchi wa mkoa wa Dar es Salaam mjitokeze kwa wingi kunufaika na fursa hii ya mkopo wa asilimia 10%ya mapato ya ndani ya Halmashauri ili muweze kujikwamua kiuchumi pia kwa wale ambao mshapata mikopo hiyo mhakikishe mnarejesha fedha hizo kwa wakati ili wengine nao waweze kupata mkopo.”

Aidha Mhe Makalla ameendelea kusema “Mimi kama kiongozi wa Serikali nimeona niwaoneshe kwamba ninaheshimu Wanawake na kuthamini juhudi zao wanazozifanya kuhusu usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake kiuchumi ambapo leo hii duniani kote wanaadhimisha siku ya Wanawake kama sisi Tanzania ambapo kitaifa hufanyika kila baada ya Miaka mitano, na Kila Mwaka kila Mkoa hufanya katika Mkoa wake lengo likiwa kuwawezesha Wanawake kujikwamua Kiuchumi, kielimu,kiafya pamoja na kuwawezesha wajasiriamali.”

Sambamba na hilo Mhe. Makalla ameweza kuzishukuru Taasisi, Mashirika na Makampuni binafsi ambayo yameweza kuwaruhusu wanawake kuweza kuungana na wanawake wengine siku hii ya leo niwaase Wanawake kuwa wamoja katika kutetea haki zenu na Taifa letu kwa ujumla na ndio maana hata mimi nimeheshimu siku hii nakuweza kuungana na ninyi.

Vilevile Mhe.Makalla aliweza kukagua mabanda ya wajasiriamali kutoka Halmashauri zote zaMkoa wa Dar es Salaam ambao ni wanufaika wa Mkopo wa asilimia 10% za mapato ya ndani ya Halmashauri ambapo aliweza kujionea bidhaa mbalimbali wanazotengeneza wanawake wajasiriamali huku akitoa rai kwa wanawake kuhakikisha wanapata mafunzo ili waweze kupata Masoko ya ndani na nje, “Kadri uchumi unavyokua fursa zinazidi kuongezeka hivyo naamini kwa mikono ya Wanawake, Masoko tunayo hivyo nitoe wito kwa wanawake wathibiti ubora wote kuwatia wanawake wengine moyo tusiwakatishe tamaa ili waweze kukua kiuchumi pia nitoe wito kwa Jamii kujenga tabia ya kununua bidhaa zinazozalishwa kwa mikono ya wajasiriamali wenzetu na pia wajasiriamali mhakikishe mnatengeneza bidhaa zinazokidhi ubora na viwango ili muweze kupata Masoko ndani na nje ya nchi.” Amesisitiza Mhe. Makalla.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Edward Mpogolo ambaye ni mwenyeji katika maadhimisho haya yaliyofanyika katika Wilaya ya Ilala amesema “Kwa niaba ya Wakuu wenzangu wa Wilaya Nyingine nipende kuwapongeza wamama wa Halmashauri zote za Mkoa wa Dar es Salaam ambao wameweza kujiajiri kupitia mkopo wa Asilimia 10% za mapato ya ndani ambapo hii leo wameweza kutambulisha bidhaa zao hivyo nipende kukushukuru Mkuu wa Mkoa Wa Dar es Salaam kwa kuungana na Wanawake hawa katika Siku yao hii Muhimu pia nikuhakikishie wakani Mimi na Wakuu wa Wilaya wenzangu tutafanya jambo kwa ajili ya kuwawezesha Wanawake hawa wajasiriamali wa Mkoa wa Dar es Salaam kujikwamua Kiuchumi.”

Akiongea kwa niaba ya Vikundi vya Wajasiriamali kutoka Mkoa wa Dar es Salaam vinavyonufaika na mikopo ya asilimia 10 %ya Halmshauri mjasiriamali wa Kikundi cha wethy kutoka Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Bibi.Letisia Pius Rutta amesema “Tunaishukuru Serikali ya Tanzania inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan katika kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapindunzi na Sera mbalimbali hasa kumuinua Mwanamke Kiuchumi ameweza kutupatia mikopo na kuanzisha majukwaa mbalimbali yanayotetea haki za Wanawake hivyo tunamuahidi tutatumia fursa hii kujikwamua Kiuchumi.”

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa wa Kidato cha Pili 2022 January 04, 2023
  • Taarifa kwa Umma kuhusu Wanafunzi kuripoti shuleni mwaka 2023 January 12, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Nne (CSEE) 2022 January 29, 2023
  • TANGAZO DHIDI YA UTAPELI WA AJIRA July 20, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Umoja wa Wajasiriamali Walemavu Dar wafanya kongamano la kumpongeza Rais Samia

    March 17, 2023
  • Wajumbe wa Halmashauri Kuu wapitisha Utekelezaji wa Ilani ya Chama katika Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kuanzia Januari 2021 hadi Disemba 2022

    March 16, 2023
  • Kamati ya Siasa Wilaya ya Ilala Yaridhishwa na utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

    March 14, 2023
  • Jiji la DSM latekeleza agizo la Waziri Kairuki kwa Shule ya Kifuru, DCB yachangia madawati 30

    March 09, 2023
  • Angalia zote

Video

NAPA
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 2128800

    Namba ya Mkononi: 0713614364

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.