• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
  • Pangisha

Kamati ya Uchumi na Huduma za Jamii Jiji la DSM yafanya ziara ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo kwa robo ya Pili ya Oktoba-Disemba, 2021

Tarehe iliyowekwa: February 14th, 2022

Na: Hashim Jumbe

Kamati ya Uchumi na Huduma za Jamii, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, leo tarehe 14 Februari, 2022 imefanya ziara ya ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo iliyotekelezwa kwa kipindi cha robo ya Pili iliyoanzia Oktoba na kuishia Disemba, 2021.


Ziara hiyo ya kawaida yenye lengo la kuwapa fursa wajumbe wa Kamati hiyo kuweza kukagua na kutolea mapendekezo Miradi ya Maendeleo iliyotekelezwa na Halmashauri kwa kipindi cha robo ya Pili katika Sekta za Elimu, Afya, Kilimo, Mifugo na Uvuvi pamoja na kufuatilia vikundi vilivyonufaika na 10% ya fedha za Mikopo inayotolewa na Halmashauri kwa vikundi vya wanawake, vijana na wenye ulemavu.


Wakiwa kwenye ziara hiyo leo, Kamati ilikagua ujenzi wa mabucha ya nyama yanayojengwa Vingunguti, kama anavyoeleza Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Steven Mushi "leo kamati tulikuwa na ziara ya kutembelea miradi ya maendeleo ambayo imefanyika katika Jiji la Dar es Salaam, tulianza na mradi wa mabucha ambao una thamani ya Shilingi Milioni 300, tumefika na tumekuta ipo katika hali nzuri teyari  kwa ajili ya matumizi na muda siyo mrefu yataanza"


Aidha, Kamati hiyo ilipata pia nafasi ya kutembelea kikundi cha usindikaji wa ndizi kinachoitwa 'Banana Group' kilichopo Vingunguti, ambapo Kamati ilijionea namna ndizi zinavyovundikwa, zinavyopokelewa na kutayarishwa mpaka zinapoiva, kikundi hicho ni moja kati ya vikundi vilivyonufaika na 10% ya Mikopo inayotolewa na Halmashauri kwa wanawake, vijana na wenye ulemavu.


Mwisho, kamati hiyo ilitembelea pia ujenzi wa Vyumba Nane (8) vya Madarasa Shule ya Sekondari Bangulo vilivyojengwa kwa fedha za UVIKO-19 pamoja na ujenzi wa matundu kumi (10) ya vyoo yanayojengwa kwa fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri.


Ziara hiyo ilitamatishwa na majumuisho ambapo Mhe. Mushi alitoa shukrani kwa Serikali ya Awamu ya Sita (6) ikiongozwa na Mhe. Rais Samia kwa kutoa fedha za miradi, Mstahiki Meya, Madiwani pamoja na timu ya wataalamu wa Jiji la Dar es Salaam "tunampongeza Mama yetu, Mhe. Samia kwa namna ambavyo anavyoachia fedha za miradi na tunaipongeza Halmashauri inavyojitahidi kwenye mapato yake ya ndani na kwenye ile 10% ya mikopo ya wanawake, vijana na walemavu"


Itakumbukwa kuwa ziara hiyo ni ya kisheria na itafuatiwa na kikao cha Kamati kwa ajili ya kujadili taarifa za utendaji kazi pamoja na kupokea taarifa ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa kipindi cha Oktoba hadi Disemba, 2021

Matangazo

  • Tangazo la upangishaji eneo la wazi katika jengo DCC Business Park (Machinga Complex) February 18, 2021
  • Orodha ya waliochaguliwa kufanya usaili utakaofanyika Karakana ya Mwananyamala tarehe 16 Februari, 2021 kwa nafasi ya kazi ya kukusanya ushuru wa maegesho yasiyo rasmi "Wrong Parking" February 15, 2021
  • Tangazo la ajira ya muda November 03, 2021
  • uchaguzi wa wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza mwaka 2022-Shule za Ilala Mjini November 24, 2021
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Baraza la Madiwani Jiji la DSM lapitisha taarifa ya utendaji kazi ya robo ya pili kuanzia Oktoba-Disemba, 2021

    March 02, 2022
  • Mkuu wa Wilaya ya Ilala amaliza mgogoro wa mpaka Mtaa wa Ngobedi 'B'

    February 21, 2022
  • Kamati ya Fedha Jiji la Dar es Salaam yakagua Miradi ya maendeleo iliyotekelezwa kwa kipindi cha robo ya pili (Octoba -Desemba, 2021)

    February 17, 2022
  • Kamati ya kudhibiti UKIMWI Jiji la DSM yatembelea vituo vinavyojishughulisha na uelimishaji wa shughuli za kudhibiti UKIMWI

    February 16, 2022
  • Angalia zote

Video

Omary Matulanga achaguliwa kuwa Mstahiki Meya Jiji la Dar es Saaam
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Wananchi

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 2128800

    Namba ya Mkononi: 0713614364

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.