• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Watendaji wa Sekta ya Elimu Jiji la DSM watakiwa kupandisha ufaulu, huku wakisaini mikataba ya uwajibikaji

Tarehe iliyowekwa: January 16th, 2023

Watumishi wa Idara ya Elimu Msingi na Idara ya Elimu Sekondari Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, leo tararehe 16 Januari, 2023 wamefanya kikao kazi cha pamoja katika ukumbi wa Shule ya Msingi Mnazi Mmoja, lengo likiwa ni kuboresha Sekta ya Elimu ili wanafunzi waweze kupata elimu katika mazingira mazuri ambayo yatapelekea kupandisha ufaulu wao.

Kikao hicho kiliwahusisha Walimu Wakuu wa Shule za Msingi za Serikali, Wakuu wa Shule za Sekondari za Serikali, Waratibu wa Elimu Kata na Maafisa Elimu kutoka Idara za Elimu za Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, ambapo Mkuu wa Wilaya ya Wilaya Ilala, Mhe. Ludigija alitumia fursa hiyo kuwataka Watendaji katika Sekta ya Elimu kufuata maelekezo yaliyoelekezwa na Serikali ikiwa ni pamoja na mahudhurio, ufundishaji na ufundishwaji kuwa na mikakati na mbinu katika kutekeleza hayo kwani lengo la Serikali ni kuhakikisha kila mtoto anakuwa Shuleni na kupata matokeo chanya.

Sambamba na hilo lakini pia Mkuu wa Wilaya ameagiza Wakuu wa Shule za Sekondari kuhakikisha Wanafunzi wote waliopangwa Katika Shule zilizopo Wilaya ya Ilala wanaripoti huku akiwapongeza Wakuu wa Shule za Sekondari kwa usimamizi mzuri wa ujenzi wa madarasa “Niwapongeze Wakuu wa Shule za Sekondari kwa usimamizi mzuri wa ujenzi vyumba vya madarasa, kwa kweli mmejitahidi kuendana na kasi na madarasa yamejengwa kwa ubora unaotakiwa” Amesema Mhe. Ludigijja.

Naye, Afisa Elimu Sekondari Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Mwl. Musa Ally amesema matarajio yao ni kuhakikisha maelekezo yote yaliyotolewa kwenye Vigezo vya Utendaji vinafikiwa kwa Asilimia 100 na kuhakikisha miundombinu katika Sekta ya Elimu kama madarasa, matundu ya vyoo, maabara, mabweni inaimarika.

Vilevile Sekta hiyo ya Elimu imejipanga kuhakikisha ufaulu katika Halmshauri hiyo unapanda kutoka asilimia 35 mpaka asilimia 50 na zaidi, wanafunzi wa Kidato cha Nne kufaulu kwa daraja la Kwanza, Pili na Tatu kwa ufaulu wa A, B, C sambamba na udahili na mahudhurio vifikie asilimia 100.

“Lengo letu ni kufanya yasiyowezekana yawezekane kwa kuhakikisha miundombinu katika Sekta ya Elimu inaimarika na mazingira mazuri yote yanayofanya mwanafunzi kuweza kusoma vizuri yanafanyika” Amesema Mwl. Mussa Ally.

Akizungumza katika Kikao hicho Afisa Elimu Msingi Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Mwl. Sipora Tenga amesema kupitia kikao hicho watahakikisha kila Afisa Elimu wa Kata na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam awajue wanafunzi wasiojua kusoma na kuandika na kuwapeleka katika hatua nzuri kulingana na Kata zao lakini pia watahakikisha Walimu wanaofundisha Darasa la Tatu wanakuwa mahiri katika somo la Kiingereza ili kuwajengea Wanafunzi wa Darasa la Tatu umahiri wa lugha ya kiingereza.

Sambamba na hayo kikao hicho pia kiliambatana na kusaini kwa mkataba wa Uwajibikaji na Utendaji Kazi kwa Maafisa Elimu Kata, Walimu Wakuu wa Shule za Msingi na Wakuu wa Shule za Sekondari ndani ya Halmshauri hiyo.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.