• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Watendaji wa Kata, Mitaa pamoja na Wenyeviti wa Mitaa wa Jiji la DSM wakumbushwa kutekeleza majukumu yao kwa Uadilifu

Tarehe iliyowekwa: June 27th, 2023

Maafisa Watendaji wa Kata, Mitaaa pamoja na Wenyeviti wa Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam wametakiwa kufanya kazi ya kuwahudumia wananchi kwa weledi kwa kuzingatia uadilifu na maadili ya Utumishi wa Umma.

Maagizo hayo yametolewa Leo Juni 27, 2023 na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Edward Mpogolo wakati wa kikao kazi cha kukumbushana majukumu ya kazi zao, maadili ya utumishi wa umma sambamba na usimamizi wa miradi inayotekelezwa katika Halmashauri kilichofanyika katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Shaaban Robert Uliopo Upanga Jijini Dar es Salaam.

Aidha Akiongea katika kikao hicho Mhe. Mpogolo amewataka Watendaji wa Kata, Mitaa pamoja na Wenyeviti wa Mitaa kuhakikisha wanafanya kazi kwa ushirikiano pamoja na kujenga mahusiano mazuri na wananchi, Madiwani pamoja na viongozi wote wa Chama cha Mapinduzi lengo likiwa ni kutekeleza Ilani ya Chama pamoja na kutambua kazi kubwa anayoifanya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan la kuhakikisha Wananchi wanapata huduma bora kwa ukaribu na uharaka zaidi.

Sambamba na hilo Mhe . Mpogolo amesema “Napenda kuwapongeza wote kwa kazi Nzuri mnazozifanya za kusimamia miradi pamoja na kuhudumia wananchi licha ya changamoto ndogondogo zinazowakabili Ila nipende kuwakumbusha mfanye kazi zenu kwa uadilifu msijihusishe na kazi za ukusanyaji wa mapato kwani sio kazi zenu hivyo mtekeleze majukumu yenu ya kuwahudumia Wananchi kwa ukaribu zaidi ili kutekeleza adhma ya Rais wetu ya kuhakikisha kila Mwananchi anapata huduma bora kwa wakati”.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Ndg. Jomaary Mrisho Satura aliweza kuwapongeza Watendaji pamoja na Wenyeviti kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuwahudumia wananchi katika maeneo yao huku akiwakumbusha kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu hasa kwa kuzingatia Sheria, Kanuni, taratibu na maelekezo maalumu ya Serikali.

“Kikao kazi hichi kina lengo la kuwakumbusha wajibu na majukumu yenu katika kusimamia mapato pamoja na utekelezaji wa miradi kwani imani yangu ni kuwa kila mtu anaomuongozo wa majukumu anayopaswa kutekeleza kila siku, kila mtu anafahamu sheria, kanuni na taratibu za kazi lakini zaidi zingatieni na kutekeleza maagizo yanayoshushwa kwenu, kwa kutoka ofisi ya Mkurugenzi, kwa kutambua kuwa mnaowajibu wa kufanyakazi kwa niaba ya Mkurugenzi katika maeneo yenu." Amesisitiza Ndg. Satura.

Akifunga Kikao hicho Mastahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Mhe. Omary Kumbilamoto amesema “Tumedhamiria kubadilisha Jiji letu hivyo fedha zinapotolewa zitumike kwa uangalifu na kwa uaminifu ili kufikia malengo hivyo tuwe waadilifu katika kusimamia utekelezaji wa miradi yetu pia kwa kushirikiana Mkurugenzi tutahakikisha tunasimamia vyema majukumu yetu ikiwa ni kusimamia vyema utekelezaji wa miradi inayotekelezwa na Halmashauri ya Jiji letu”.

Hata hivyo Maafisa Watendaji hao, wameushukuru uongozi wa Halmashauri kwa kikao kazi hicho chenye tija na kuahidi kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia sheria kanuni na taratibu za Utumishi wa Umma ili kufikia malengo ya Serikali ya kuwahudumia wananchi katika maeneo yao.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.