• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Wananchi Wahamasishwa Matumizi ya Nishati safi ya Kupikia

Tarehe iliyowekwa: September 27th, 2024

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira anayeshughulikia masuala ya Mazingira Bi.Christina Mndeme ametoa wito kwa mama lishe na Baba lishe  kuokoa maisha yao kwa  kutumia nishati safi ya kupikia ambayo itawaepusha na athari katika mfumo wa upumuaji pamoja na utunzaji  wa mazingira.

Bi.Mndeme ameyasema hayo leo, Septemba 27, 2024 Jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya ugawaji wa majiko ya kupikia kwa mama na baba lishe wa Kisutu iliyoandaliwa na Kampuni ya Bakhresa yenye lengo la  kuunga mkono jitihada za Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan  katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Akizungumza katika hafla hiyo Bi. Mndeme amesema, Rais Samia licha ya kuwa kinara wa Afrika kwenye kampeni ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia, pia amedhamiria kuwaondoa kina mama na baba lishe wa Tanzania katika matumizi ya nishati isiyo safi na pia kuboresha hali zao kwa kutumia nishati safi ya kupikia ambapo hii inaendana na kampeni ya kumtua mama kuni kichwani.

‘‘Nipende kupongeza sana Makampuni ya Bakhera kwa kuibeba ajenda hii ya nishati safi ya kupikia kwani mmeonesha kwa vitendo kuhakikisha mnamuunga mkono Rais wetu katika kuhakikisha tunatunza mazingira kwa kutumia nishati safi ya kupikia ambayo itaepusha athari zote za kimazingira zitokanazo na matumizi ya nishati isiyo safi, hivyo nitoe wito kwa wadau wengine kuhakikisha wanashirikiana na sisi katika kutunza mazingira ili hadi kufikia mwaka 2034 asilimia 80% ya watu wawe wanatumia Nishati safi ya kupikia."

Sambamba na hilo, Bi. Mndeme ameeleza kuwa matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa ujumla itaondoa uharibifu wa mazingira ambapo jamii itaachana na ukataji wa miti ovyo pamoja na kumtua mama kuni kichwani kwa kuwauondolea wanawake kutumia muda  mwingi katika kutafuta kuni badala yake kufanya shughuli za Kiuchumi.

Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Bi. Theresia Denis ameishukuru Kampuni ya Bakhressa kwa kuunga mkono juhudi za Mhe. Rais za kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia huku akieleza kuwa Jiji la Dar es Salaam litaendelea kuwa mstari wa mbele kuhakikisha wananchi wake wanatimia nishati safi ya kupikia ili kuondokana na athari za kimazingira na kuendelea kulinda mazingira na afya kwa ujumla.

Naye Meneja wa Uhusiano na Mawasiliano wa Makampuni ya Bakhressa Bi. Rehema Salim ameeleza kuwa katika kurudiasha fadhila kwa jamii Kampuni ya Bakhresa imeona ni vyema kuunga mkono  juhudi za Mheshimiwa  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassani za matumizi ya nishati safi ya kupikia ambapo wameanza kwa kugawa majiko 60 kwa mama lishe na baba lishe wa Kisutu huku akieleza kuwa kampeni hii ni endelevu na itafanyika nchi nzima.

Aidha, mkakati wa matumizi ya nishati safi ya kupikia, ulizinduliwa na Rais Samia Suluhu Hassan, Mei 8, 2024 ukilenga kuepuka athari za matumizi ya kuni na mkaa unaoambatana na utunzaji wa mazingira.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.