• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Kamati ya Uchumi na Huduma za Jamii Jiji la DSM yakagua Miradi ya Maendeleo iliyotekelezwa kwa kipindi cha robo ya kwanza Julai - Septemba, 2023

Tarehe iliyowekwa: October 24th, 2023

Kamati ya Uchumi na Huduma za Jamii Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, leo tarehe 24 Oktoba , 2023 wamefanya ziara ya ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo iliyotekelezwa na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa kipindi cha robo ya kwanza ya Mwaka wa Fedha 2023/2024 (Julai hadi Septemba 2023.)

Wakiwa kwenye ziara hiyo, Kamati iliweza kutembelea na kukagua miradi minne (4) ikiwemo ujenzi wa Madarasa ya ghorofa Shule ya Sekondari Mnazi Mmoja, ujenzi wa uwanja wa Mpira Shule ya Sekondari Benjamini Mkapa, ujenzi wa Madarasa 8 na matundu 13 ya Vyoo Shule ya Sekondari Jangwani pamoja na ujenzi wa Shule Mpya ya Msingi Boma.

Aidha, ujenzi wa  madarasa 20 ya ghorofa 4 Shule ya Sekondari Mnazi Mmoja mmoja uliogharimu takribani shilingi Milioni 540 ikiwa kwenye hatua ya Frame work na hadi kukamilika utagharimu shilingi bilioni 1.8, Ujenzi wa Madarasa 8 na Matundu 13 ya Vyoo Shule ya Sekondari Jangwani yenye thamani ya shilingi milioni 199.4 Fedha kutoka kwa wafadhili Barrick Gold Mine ikiwa mchango wao wa kurudisha hisani kwa jamii mbapo Madarasa nane (8) yaliyogharimu shilingi milioni 176 yakiwa yamekamilika huku matundu 13 ya vyoo yenye thamani ya shilingi  milioni 23.4 yakiwa katika hatua ya ukamilishaji pia ujenzi wa Shule ya Msingi Boma Mpya yenye madarsa sita (6) ya Msingi na Madarasa mawili (2) ya awali, jengo moja (1) la utawala na matundu kumi na sita (16) ya vyoo uliogharimu shilingi milioni 306.9 Fedha kutoka Mradi wa Boost ukiwa umekamilika huku ujenzi wa uwanja wa mpira Shule ya Sekondari Benjamini Mkapa unaotekelezwa kwa Fedha za Mapato ya Ndani ya Halmashauri ukiwa umefikia asilimia 35% ya utekelezaji ambapo hadi kufikia Disemba 31, 2023 mradi huo utakuwa umekamilika na utagharimu shilingi milioni 989.8.

Naye, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Saady Khimji akifanya majumuisho ya ziara hiyo amesema, "Leo tumetembelea baadhi ya miradi inayosimamiwa na kutekelezwa na Halmashauri ya Jiji la DSM ambapo tumeweza kuridhishwa na utekelezaji huo hivyo nitoe wito kwa watendaji wa Halmashauri kusimamia miradi hii kwa ukaribu zaidi na Sisi kama wasimamizi tutaendelea kushirikiana nao kuhakikisha miradi hii inatekelezwa kwa wakati na thamani ya Fedha inayotumika inalingana na ubora wa miradi."

Sambamba na hilo Mhe. Khimji ameendelea kusema, "Kamati hufanya ziara hizi kwa lengo la kukagua na kuhakikisha fedha zinazotolewa na Serikali Kuu pamoja na Halmashauri zinawafikia walengwa na kufanya kazi kama ambavyo wao wamepitisha kupitia vikao vya Madiwani na kuangalia thamani ya fedha hizo na kazi zinazofanyika hivyo naomba mapungufu yaliyoonekana kwenye miradi hiyo yashughulikiwe kwa wakati na kuweza kufikia hitimisho sahihi kwani tunachohitaji wananchi wote wafikiwe na huduma muhimu na bora kwa wakati kama Mheshimiwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania anavyoonesha juhudi zake katika kuwahudumia Wananchi.”

Aidha, Wajumbe wa Kamati wameridhia kuwa endapo kutakua na changamoto wakati wa utekelezaji wa miradi ni vyema changamoto hizo zikawasilishwa sehemu husika mapema na kufanyiwa kazi ili maendeleo ya wananchi yasikwamishwe huku wakiagiza miradi yote ya madarasa ya Boost yatembelewe ili kukagua kama kuna changamoto na zifanyiwe marekebisho kabla madarasa hayo hayajaanza kutumika.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.