• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Jiji la DSM latekeleza Sera ya utoaji huduma ya Chakula na Lishe mashuleni

Tarehe iliyowekwa: February 6th, 2023

Suala la usomaji shuleni linahitaji wanafunzi kuwa na afya bora na utimamu wa akili, hivyo wanafunzi wakipata chakula shuleni itawasaidia kujenga afya bora na hivyo kumudu kuelewa yale wanayojifunza shuleni na kufanya matokeo yao na ufaulu kwa ujumla kuwa wa juu.

Mnamo tarehe 29 Octoba, 2021 Serikali kupitia Wizara ya Elimu na Teknolojia ilizindua muongozo wa kitaifa wa utoaji wa huduma za chakula na lishe kwa wanafunzi mashuleni wenye lengo la kuwaelekeza wadau wa elimu nchini kote namna bora ya kutekeleza utoaji wa huduma ya chakula na lishe mashuleni.

Katika Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Muongozo huo umepokelewa kwa muitikio chanya kwani shule nyingi zimeanza kutoa huduma ya chakula mchana na kuwawezesha wanafunzi kuzingatia masomo yao kikamilifu. Shule ya Sekondari Jamhuri ni moja ya shule ambazo zimeanza kutoa huduma ya chakula kwa wanafunzi wake. Na kutokana na maelezo ya Mkuu wa shule hiyo Mwl. Boniphase Mwalwego amesema kuwa kuanzishwa kwa huduma ya chakula katika shule yake kumesaidia sana hali ya ufaulu kuwa juu hasa kwa wanafunzi wa kidato cha pili na kidato cha nne waliofanya mitihani yao ya Taifa mwaka jana wa 2022.

“Asilimia 75 ya wanafunzi wa kidato cha pili katika shule yetu wamepata ufaulu wa daraja la kwanza, na katika wanafunzi wote waliofanya mtihani huo hakuna aliyerudia kidato. Kwa upande wa Kidato cha nne asilimia 80 ya wanafunzi waliofanya mtihani huo wamepata daraja la kwanza.” Amesema Mwl. Mwalwego

Aidha amesema kuwa huduma ya chakula na lishe mashuleni inasaidia kujenga akili za wanafunzi kikamilifu. Kwa sababu hivi sasa wanafunzi wanaojiandaa na mitihani wanaanza masomo yao saa 1 asubuhi, hivyo sio rahisi kwa wao kupata chakula nyumbani kabla ya kwenda shule. Kupata chakula shuleni kunawasaidia wanafunzi kuwa wasikivu na kuzingatia kile wanachofundishwa wawapo darasani na mazingira ya shule kwa ujumla.

Vilevile utoaji wa chakula umepunguza kasi ya utoro kwa wanafunzi na kuwapa motisha ya kusoma. Hapo awali wanafunzi walikuwa na tabia ya kutoroka kabla ya vipindi kuisha kutokana na njaa, lakini kufuatia kuanzishwa kwa huduma ya chakula katika shule yao, wanafunzi wamekuwa wakihudhuria vipindi vyote darasani na kuachana na tabia ya utoro.

Mwl. Mwalwego pia amesema kuwa kwa miaka inayoendelea ana Imani kuwa uanzishwaji wa utoaji wa huduma ya chakula na lishe mashuleni utaongeza hali ya ufaulu zaidi kwa wanafunzi wao kwani akili zao zinajengeka kwa kupata lishe kwa wakati katika muda wote wawapo katika mazingira ya shule.

Sambamba na hilo wanafunzi wa shule hiyo wametoa shukrani zao za dhati kwa Serikali kwa kuanzisha muongozo huu wa chakula na lishe mashuleni, kwani umekuwa ni chachu kubwa na umesaidia kuleta hamasa kwa wanafunzi katika mchakato mzima wa kusoma na kujifunza.

Ikumbukwe kuwa moja ya vitu ambavyo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan amevipa kipaumbele ni suala la Lishe bora nchini. Na hii ikiwa ni mkakati wa kuhakikisha nchi inaondokana na tatizo la utapiamlo na wananchi wake wanakuwa na afya bora na kuwawezesha kufanya kazi kwa bidi kwa maslahi mapana ya mwananchi mmoja mmoja na Taifa zima kwa ujumla.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.