• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Jiji la DSM kufanya kazi kikanda

Tarehe iliyowekwa: July 19th, 2023

Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam leo Tarehe 19 Julai, 2023 imetoa taarifa kwa Umma na wadau kwa ujumla kupitia vyombo vya habari kuwa,imegawanya eneo la Jiji katika kanda za kiutawala ili kurahisisha utoaji wa huduma unaolenga kutoa huduma zenye ubora na usawa kwa jamii kwa kuzingatia utawala bora na kutumia kikamilifu rasilimali zilizopo.

Akitoa taarifa hiyo katika ukumbi wa mikutano wa Arnatoglou uliopo Mnazi Mmoja Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Bi.Tabu Shaibu amesema kuwa kuanzishwa kwa huduma za Kanda kutaongeza wigo wa ukusanyaji wa Mapato kwa kuwa ufuatiliaji wa walipa kodi utafanyika kwa ukaribu na ufanisi na kuiwezesha Halmashauri kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.

Vilevile amesema kuwa kutasaidia kuweka mipango itakayozingatia mahitaji maalum ya maeneo tofauti kwa kuwa kila eneo linaweza kuwa na changamoto na mahitaji yake ya kipekee ,kugawa maeneo kutawezesha kubuni na kutekeleza programu zitakazozingatia mahitaji ya kila eneo.

Aidha ameongeza kuwa mpango huu utarahisisha ufanisi na usimamizi wa utoaji huduma kwa kuwa na eneo dogo ambapo kutasaidia kuimarisha usimamizi wa huduma za Umma na kusababisha utendaji kazi ulio bora na uwezo wa kurekebisha kwa haraka changamoto zinazojitokeza hivyo kuimarisha utekelezaji mzuri wa bajeti na mipango ya maendeleo.

Amesema, “Kuwepo kwa kanda kutasaidia kusikiliza na kutatua changamoto mbalimbali za wananchi kwa wakati kwa kuwa wakati mwingine matatizo ya wananchi yanashindwa kutatuliwa kwa wakati kwa sababu ya umbali wa kuzifikia huduma wanazozihitaji”

Bi. Tabu amesema kuwa kutakuwa na jumla ya Kanda 7 za kutolea huduma ambapo Kanda namba 1 ina Kata za Kivukoni, Kisutu, Upanga Mashariki na Upanga Magharibi na Ofisi ya Kanda itakuwa katika ofisi ya Kata Upanga Mashariki.

Kanda namba 2 ina Kata za Ilala, Mchikichini, Jangwani, Kariakoo, Gerezani na Mchafukoge, Ofisi ya Kanda itakuwa katika ofisi ya Kata Gerezani.

Kanda namba 3 inahusisha Kata za Buguruni, Mnyamani, Vingunguti, Kipawa, Minazi Mirefu na Kiwalani. Ofisi ya Kanda itakuwa katika Ofisi ya Kata ya Mnyamani .

Kanda namba 4 itajumuisha Kata za Tabata, Liwiti, Kimanga, Kisukulu, Segerea, Bonyokwa na Kinyerezi. Ofisi ya Kanda itakua katika Ofisi ya Kata ya Kinyerezi.

Kanda namba 5 itakuwa na Kata za Ukonga, Gongo la Mboto, Pugu Stesheni na Pugu na Ofisi ya Kanda hii itakuwa katika Ofisi ya Kata ya Gongo la Mboto.

Kanda namba 6 ina Kata za Kitunda, Mzinga, Kivule, Kipunguni na Majohe ambapo wananchi wa Kata hizi watahudumiwa katika Ofisi ya Kata ya Kipunguni.

Kanda namba 7 inahusisha kata za Buyuni, Chanika, Zingiziwa na Msongola ambapo Ofisi ya Kata ya Chanika itatumika kama Ofisi ya Kanda hii.

Vituo hivi vya kanda tayari vimekwishaanza kutoa huduma chini ya Uongozi wa Mameneja wa Kanda.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.