• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

DC Mpogolo awataka walimu wa mkataba kuzingatia nguzo za Utumishi wa Umma

Tarehe iliyowekwa: April 16th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mh. Edward Mpogolo amewataka walimu wa ajira za mkataba walioajiriwa na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kuzingatia nguzo 5 za utendaji, na kuwa wazalendo kwa Nchi katika kipindi chote cha utekelezaji wa majukumu yao.

Hayo ameyasema Leo tarehe 16 Aprili, 2024 katika kikao kilichojumuisha Maafisa Elimu Kata, Wakuu wa Shule na walimu wa ajira za mkataba katika Ukumbi wa Arnatoglou kwa lengo la kuwaasa na kuwaelekeza walimu wa mkataba yale wanayopaswa kwenda kuyafanya wakiwa kazini. 

Akiongea na walimu wa mkataba Mhe. Mpogolo amesema “Natoa pongezi kwa walimu walioajiriwa na Halmashauri yetu, nawaasa muitumie nafasi hii mliyoipata kwa kuishi katika nguzo 5 ambazo ni kujua jukumu lako kwa watoto, kujifunza kuishi na kuendana na jumuiya inayokuzunguka, kujua mwajiri wako anataka nini, kujua jukumu lako kama mwalimu, na kujua wajibu kwa Taifa lako. Pia nawaomba mkaongeze juhudi na bidii katika ufundishaji ili kupandisha ufaulu katika shule ili Jiji letu liendelee kuwa kinara katika Elimu."

Aidha, Akiongea katika kikao kazi hicho Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Mhe. Omary Kumbilamoto amempongeza Mkuu wa Wilaya ya Ilala kwa jitihada anazozifanya za kuboresha Elimu katika Jiji la Dar es Salaam huku akimuhakikishia kutekeleza yale yote aliyoyaagiza.

Naye, Kaimu Afisa Elimu Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Bi. Doreen Masawe ameeleza kuwa “Nipende kumshukuru Mkurugenzi wa Jiji kwa kuajiri walimu 150 wa mkataba katika masomo ya sayansi kwani kutokana na ajira hizo changamoto ya ufaulu katika masomo ya sayansi itakua imetatuliwa kwa kiasi hivyo Nipende kuwahakikishia kupitia ajira hizi ufaulu utazidi kuongezeka zaidi katika Halmashauri yetu."

Aidha, akimwakilisha Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Bi. Fidea Mapunda amewakumbusha walimu wajibu wao katika kuhakikisha wanafanya kazi kwa uadilifu kwa kutimiza majukumu yote ya kitaifa na kijamii kwa kuwalea watoto kwa maadili ya kinidhamu pamoja na kuzingatia sheria na kanuni za Utumishi wa Umma ikiwemo utoaji wa huduma Bora bila upendeleo, pamoja na kufanya kazi kwa bidii na kwa wakati katika ubora unaotakiwa kwani walimu ndio kioo cha maadili nchini ambapo kwa kuzingatia hayo  sekta ya Elimu nchini itazidi kuimarika.

Akiongea kwa niaba ya Afisa udhibiti ubora wa Shule Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Bi. Pudensiana Justine Kisela abeles kuwa “Kikao hichi ni muhimu sana kwenu katika kuhakikisha sekta ya elimu katika Halmashauri yetu inakua kwa kasi hivyo niwaase Waalimu muwe wabunifu kuwajengea wanafunzi uwezo mkubwa wa kufikiri na sio kukariri tu kwaajili ya mitihani. Pamoja na hayo nitoe wito kwa Wakuu wa Shule kuhakikisha mnasimamia walimu wengine kutumia zana za kazi pamoja na kuandaa azimio la kazi Ili kuandaa andalio la somo kama Wizara inavyoelekeza lengo likiwa ni kuleta wepesi wakati wa kufundisha."

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.