• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

DC Ilala asisitiza upatikanaji wa haki za wazee katika kupata Huduma za Afya

Tarehe iliyowekwa: October 13th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Edward Mpogolo asisitiza upatikanaji wa haki za wazee katika kupata huduma za afya hayo ameyasema leo Oktoba 13, 2023 wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniani yaliyofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja yaliombatana na kauli mbiu isemayo ‘Uthabiti wa Wazee kwenye Dunia yenye Mabadiliko’.

Akiongea wakati wa hafla hiyo Mhe. Mpogolo ameeleza kuwa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya kwa kushirikiana na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam watazingatia haki za wazee na wananchi wote wanaowahudumia.

“Sisi kama sehemu ya huduma kwa Watanzania tutahakikisha tunazingatia haki kwa wazee na watu wote tunaowahudumia kama Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anavyotaka na tutahakikisha tunaboresha huduma za afya kwa wazee wetu kwa kuwapatia kadi za matibabu pamoja na upatikanaji wa dawa hivyo nitoe wito kwa Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kuhakikisha dawa muhimu za magonjwa yanayowasumbua wazee zipo katika vituo vyote vya kutolea huduma za afya ili wapate matibabu ya uhakika katika vituo hivyo kwani Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amewekeza zaidi ya Shilingi Bilioni 20 kaajili ya uboreshaji wa huduma za afya na miundombinu hivyo tuhakikishe tunaunga mkono juhudi zake."

Sambamba na hilo Mhe. Mpogolo alikabidhi vitambulisho 360 vya bima ya ICHF kwa waze huku akiwaahidi wazee kuwa wavumilivu kwani Halmashauri itaendelea kutoa vitambulisho vya matibabu kwa ajili yao sambamba na kumuagiza Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kuona namna gani wazee watashirikishwa kuhudhuria vikao vya baraza.

Awali akitoa taarifa ya usimamizi na uratibu wa shughuli za dawati la wazee kwa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Mratibu wa dawati la Wazee Bi. Millen Makundi ameeleza kuwa dawati la wazee limekua likitekeleza majukumu yote kwa mujibu wa Sera ya Taifa ya Mwaka 2003 yenye mpangomkakati wa kuzuia na kupambana na mauaji ya wazee Tanzania pamoja na kutekeleza sera ya misamaha ya matibabu kwa wazee wenye umri wa miaka 60.

Aidha Bi. Makundi ameeleza kuwa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ina jumla ya wazee 21,175 kati yao wanaume 10,058 na wanawake 11,117 ambapo wazee 18,613 wamepewa vitambulisho huku wazee 2345 wakiweza kupatiwa bima za afya za ICHF.

Akitoa shukrani zake kwa Mkuu wa Wilaya ya Ilala pamoja na viongozi wote wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Baraza la wazee Wilaya ya Ilala Bw. Salim Matimbwa ameshukuru uboreshwaji wa huduma za matibabu kwa wazee huku akiomba ofisi ya Mkurugenzi kushirikishwa kwenye baraza la madiwani pamoja na vikao vingine vinavyohitaji ushiriki wa wazee.

Maadhimisho haya Kitaifa yamefanyika tarehe 06 Oktoba 2023 Mkoani Geita huku kwa upande wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam yakifanyika Leo Oktoba 13 yakiwa yameambatana na Siku ya Macho Duniani yenye kauli mbiu isemayo ‘Penda Macho yako mahali pa kazi’ sambamba na siku ya watu wenye ugonjwa wa akili na kauli mbiu isemayo ‘Afya ya Akili ni haki kwa binadamu wote’

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.