• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Utalii

UTALII KATIKA MKOA WA DAR ES SALAAM

Mkoa wa Dar es Salaam ni muhimu sana katika   uchumi wa Tanzania. Unapatikana katika pwani ya Bahari ya Hindi na una Bandari kubwa katika Afrika mashariki unaoufanya mkoa huu kuwa mashuhuri sana kiuchumu. Una miundombinu ya uhakika ambayo ni barabara nzuri za lami, hoteli zenye hadhi ya kuanzia nyota 1 hadi  5 na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa ujulikanao kama (Mwalimu Nyerere International Air Port). Uwepo wa Bandari kubwa na ya kisasa unaufanya Mkoa uweze  kufikika kirahisi kwa kupitia Baharini na Nchikavu kutoka katika kila pembe ya Dunia na kuwa kiungo muhimu katika Sekta ya Utalii.

Mkoa wa Dar es Salaam hauko nyuma katika Sekta ya utalii. Mkoa huu una vivutio vingi ambavyo ni muhimu katika kuvutia watalii. Vivutio vya asili vilivyopo katika Mkoa wa Dar es Salaam ni Bahari yenye fukwe nzuri, Misitu ya Mikoko na Miyombo, Visiwa, Matumbawe na hifadhi ya wanyama Dar es Salaam zoo.

Dar es Salaam ina uoto wa asili wa aina mbili ambao ni Misitu ya Mikoko yenye ukubwa wa hekta 2760 na Miyombo yenye ukubwa wa hekta 1380.  Misitu ya Mikoko inapatikana katika mwabao wa Bahari ya Hindi na Misitu ya Miyombo inapakika katika maeneo ya uwanda wa juu. Misitu hii imehifadhiwa kwa ajili ya makazi na mazalia ya viumbe wa baharini na nchi kavu na ni kivutio kizuri cha utalii katika mkoa wetu.

Uwepo wa Bahari ya Hindi katika Mkoa huu ni kivutio kizuri sana cha utalii kwa kutoa muonekano unaovutia na kuleta upepo mzuri. Bahari inaweza kutumika kwa kufanya mashindano ya kuendesha boti pamoja na kuogelea. Bahari vilevile ni hifadhi ya samaki wengi wanaovutia. Ufukwe mzuri wa Koko wenye eneo kubwa la kupumzika ni kivutio kizuri cha utalii kwa wenyeji na wageni

Mkoa vilevile una visiwa vikubwa vitatu vilivyo umbali kidogo kutoka katika ufukwe wa Bahari. Visiwa hivyo ni  Mbudya, Bongoyo na Pangavini. Visiwa hivi vina misitu mikubwa ya asili inayopendesha mazingira na ni makazi ya viumbe wa nchi kavu kama vile ndege na nyoka. Vimezungukwa na miamba ya matumbawe (coral reefs) ya rangi mbalimbali na ni mazalia ya samaki.

Mkoa huu una vivutio vingi vya kale ambavyo ni mabaki ya tokea Utawala wa Mwarabu, Mjerumani na Muingereza pamoja na mabaki ya zana na watu wa kale. Mabaki haya yanaonekana kama alama zilizopo ardhini na kwenye majengo.

  • Makumbusho ya Taifa yanayoonesha mabaki ya mafuvu ya binadamu wa kale pamoja na nyayo kutoka katika mapango maarufu ya Olduvai, Hifadhi ya zana za kale za uhunzi pamoja na picha za asili ya makabila mbalimabali.
  • Kijiji cha Makumbusho ni kivutio kizuri cha utalii kinachoonesha tamaduni za makabila yasipungua 100 ya Tanzania. Kinazo nyumba za asili zilizojengwa kwa tope na kuezekwa kwa nyasi na tope. Vivevile kina michoro ya asili, mikeka iliyosukwa kwa mikono na ngoma za asili zinazovutia kucheza.
  • Kunduchi Beach yenye mabwawa makubwa ya kuogelea pamoja na Uwanda mkubwa wa Bahari unaotumika kwa michezo ya kukimbizana kwa pikipiki za majini ni kivutio kikubwa cha utalii katika Mkoa wetu. Katika hoteli hii kuna maeneo yaliyotengenezwa kwa ajili ya michezo ya watoto na migahawa ya vyakula ambavyo hutia hamasa kutembelea maeneo haya.
  • Vivutio vingine mbalimbali vinavyobeba historia ya ukoloni kuanzia Utawala wa Mwarabu hadi Muingereza ni uwepo wa nyumba za ibada kama vile Msikiti wa Mtoro na Nyamwezi iliyopo Kariakoo, Kanisa  (St. Joseph’s, The White Father’s Mission House), 
  • Ikulu Ofisi kuu ya Utawala wa nchi hii yenye usanifu wa kale iliyopambwa na ndege wazuri wasiopatikana eneo lolote Duniani kivutio kizuri cha utalii katika mkoa wetu.
  • Vilevile Mkoa unatambulika kwa kuwa na hoteli zenye hadhi ya nyota tano ambazo zinatoa uhakika wa malazi salama kwa watalii.

Ushirikiano na Miji mingine ya Utalii Duniani ni jambo muhimu sana, tunaweza kuibadilisha Dar es Salaam kuwa Jiji kuu la Utalii Duniani na kuliongezea Taifa kipato. Si hivyo tu bali uchumi wa watu utabadilika na kupunguza umasikini. Kwa kuzingatia kwamba Serikali yetu inasisitiza mabadiliko katika kuboresha uchumi wa viwanda ili kuondoa umasikini na kufikia malengo ya kuwa na uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.

 

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.